utt

.

line

line

line of success

line of success

Thursday, July 2, 2015

CHADEMA YAGARAGAZWA NA CCM KESI ZA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Mahakama ya Wilaya ya Iringa imetoa hukumu ya kutengua matokeo ya mitaa 13 kutoka Manispaa ya Iringa ili kufanya uchaguzi wa marudio wa Serikali za Mitaa kutokana na kasoro kadhaa zilizojitokeza katika uchaguzi uliofanyika Desemba 14 mwaka 2014.

Hukumu hiyo ilitolewa jana mbele ya mahakamu wakazi wanne ambao ni Andrew Scout, John Mpitanjia, E. Nassoro na Isaya, waliokuwa wanaendesha kesi hizo katika Mahakama ya Wazi ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Iringa.

Chama cha Mapindizi (CCM) kulifungua kesi 35 za madai za uchaguzi wa serikali za mitaa tarehe 13.01.2015 na kuwakilishwa na wakili msomi, Gaster Likatage Mdegela dhidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na chama wananchi CUF, ambapo kesi 34 zilikuwa za Chadema na kesi moja tu ndio ilikuwa ya CUF.

No comments:

Post a Comment