Mahakama
ya Wilaya ya Iringa imetoa hukumu ya kutengua matokeo ya mitaa 13
kutoka Manispaa ya Iringa ili kufanya uchaguzi wa marudio wa Serikali
za Mitaa kutokana na kasoro kadhaa zilizojitokeza katika uchaguzi
uliofanyika Desemba 14 mwaka 2014.
Hukumu
hiyo ilitolewa jana mbele ya mahakamu wakazi wanne ambao ni Andrew
Scout, John Mpitanjia, E. Nassoro na Isaya, waliokuwa wanaendesha kesi
hizo katika Mahakama ya Wazi ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Iringa.
Chama
cha Mapindizi (CCM) kulifungua kesi 35 za madai za uchaguzi wa serikali
za mitaa tarehe 13.01.2015 na kuwakilishwa na wakili msomi, Gaster
Likatage Mdegela dhidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na
chama wananchi CUF, ambapo kesi 34 zilikuwa za Chadema na kesi moja tu
ndio ilikuwa ya CUF.
No comments:
Post a Comment