Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete anatarajiwa kufunungua Maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam
(DITF) hapo kesho Julai mosi. Maonyesho hayo yaliyoanza Juni 28,
yatafikia kilele Julai 7 na yanatarajiwa kukuza sekta ya uwekezaji
kutokana na ushiriki wa nchi nyingi. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa
TanTrade, Jacqueline Maleko amesema nchi 25, kampuni za nje 400 na ndani
1,700 zinatarajiwa kushiriki kwenye maonyesho haya. Ameongeza kuwa
maonyesho hayo ni fursa nzuri kwa wananchi na wafanyabiashara kukutana
na wenzao kutoka mataifa mengine. Katika hatua nyingine amesema kuwa
Julai 3, itakuwa siku maalumu kwa wanafunzi kuanzia wa shule ya awali,
msingi, sekondari na vyuo vikuu na wataingia kwa makundi na kupata
punguzo la kiingilio badala ya kulipa Sh4,000 watalipa Sh1,000.
No comments:
Post a Comment