utt

.

line

line

line of success

line of success

Wednesday, June 17, 2015

Waziri Mmarekani amuuliza JK utitiri wa wagombea urais

Dar/Mikoani. Waziri Mdogo wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeongoza Kitengo cha Masuala ya Afrika, Linda Thomas-Greenfield amemuuliza Rais Jakaya Kikwete iwapo ana mtu wake katika orodha ndefu ya makada waliojitokeza kuomba kuwania urais kwa tiketi ya CCM.
Waziri huyo aliuliza swali hilo usiku wa kuamkia Jumatatu (Juni 14, 2015) mjini Johannesburg, Afrika Kusini wakati anazungumza na Rais Kikwete kutokana na wanachama wa CCM 35 kujitokeza kuchukua fomu za kuwania urais.
Viongozi hao walikuwa wanahudhuria Mkutano wa 25 wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika, kwa siku mbili, kwenye Kituo cha Mikutano cha Sandton Convention jijini Johannesburg, Afrika Kusini na kumalizika jana.
Makada hao wa CCM wameibua upinzani mkali kwenye mbio za urais na hadi sasa hakuna dalili za mtu yeyote kuwa ana nafasi kubwa ya kupitishwa, hali ambayo imesababisha vyombo vya habari kubashiri kuwa mteule wa CCM anajulikana kwa viongozi wa juu wa chama hicho tawala.
Wakati nchi ikijiandaa kupata kiongozi mpya atakayeongoza Serikali ya Awamu ya Tano, mbio za urais ndani ya CCM zimevutia idadi kubwa ya wanachama ambayo haijawahi kutokea kabla na baada ya kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini mwaka 1992 baada ya watu 35 kuchukua fomu hadi sasa.
Mwaka 1995, wanaCCM waliojitokeza kutaka kumrithi Rais Ali Hassan Mwinyi walikuwa 15 na mwaka 2005 waliojitokeza kutaka kumrithi Rais Benjamin Mkapa walikuwa 11.
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ilisema jana kuwa mwanzoni tu mwa mazungumzo baina ya viongozi hao, Linda alimuuliza Rais Kikwete, “Je, unaye mgombea yeyote ambaye unampendelea miongoni mwa utiriri wa wagombea”.
Baada ya swali hilo, kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, Rais Kikwete alijibu, “Sina mgombea ninayempendelea. Wagombea wote ni wa kwangu, ni wa chama changu, isipokuwa ninayo kura moja ambayo kwa mujibu wa taratibu za haki katika chama chetu nitaitumia katika vikao mbalimbali”.
Kuhusu utiriri wa wagombea, Rais Kikwete alisema wingi wa wagombea ni jambo zuri kwa CCM.
“Hiki ni chama kikubwa. Wingi unatupa nafasi ya kujadili kwa nafasi nani awe mgombea wetu. Isitoshe, tunaona wagombea wengi zamu hii kwa sababu ya wigo mkubwa wa uhuru ambao umejengeka katika nchi yetu katika miaka ya karibuni.
“Vile vile, wingi wa wagombea unathibitisha mafanikio yetu katika miaka 10 iliyopita kwa sababu tungeshindwa, watu wangeogopa kujitokeza kugombea nafasi hiyo.”
Rais Kikwete alisema hana tatizo na wingi wa wagombea kwa sababu haiwezekani kuwazuia watu kugombea nafasi hiyo kwa sababu ni haki yao.

No comments:

Post a Comment