utt

.

line

line

line of success

line of success

Wednesday, June 17, 2015

Profesa Sospeter Muhongo ni miongoni mwa makada wa CCM waliochukua fomu za kuomba kuteuliwa kuwani kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao.  Katika makala haya mwandishi anazungumza na watu walio karibu na kada huyo wa CCM, ambaye alijiuzulu wadhifa wa Waziri wa Nishati na Madini katika kashfa ya wizi kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, kabla hajasafishwa baadaye kwamba hahusiki.
Shemejji yake amsifu kwa uadilifu
“Wanaomtuhumu Profesa Muhongo kuhusu ufisadi hawamfahamu. Huyu ni kati ya warithi sahihi wa Mwalimu Nyerere, inapofikia suala la uadilifu na kutotumia cheo kujinufaisha,” anaanza kueleza Bertha Mtaragara, shemeji mkubwa wa Profesa Muhongo.
Mtaragara anasema kwa tuhuma za ufisadi zilipoibuka dhidi ya Profesa Muhongo, familia ilishtuka na kufadhaika kupita kiasi kwa sababu inajua tabia yake kuwa siyo fisadi, mla rushwa wala mpenda maslahi binafsi.
“Binafsi nilimpigia simu na kumuuliza ukweli wa jambo hilo iwapo kweli amehusika. Aliponisisitizia na kunithibitishia hajausika nikamsisitiza amwachie Mungu kwani ndiye mwamuzi wa haki. Na hakika ukweli umedhihiri baada ya uchunguzi kuwa hakuhusika,” anasema Mama Mtaragara na kuongeza:
“Tunaomfahamu Muhongo tangu utoto hatuamini kama kweli anaweza kubadilika kiasi cha kufikia hatua ya kuibia jamii yake ili ajinufaishe binafsi kwa sababu siyo tabia yake,”
Anasema familia ililazimika kufunga na kuomba kashfa ya Escrow ilipoibuka ili ukweli ubainike iwapo Profesa Muhongo alihusika au la.
“Baada ya suala la Escrow kumalizika, familia nzima akiwemo Profesa Muhongo na mkewe Bertha, tulienda nyumbani kwa kaka mkubwa wa familia Kingi Musiba kufanya ibada ya kumshukuru Mungu,” anabainisha Mama Mtaragara.
Tabia ya Muhongo tangu utoto
“Kusema ukweli bila kujali mhusika wala madhara yanayoweza kumkuta kwa kuusema ukweli huo ni moja kati ya sifa na tabia ya Profesa Muhongo tangu utoto,” anasema Mama Mtaragara
“Hakuwahi na ninaamini hatakuwa na tabia ya kufurahisha watu kwa maneno ya sifa bandia. Wakati mwingine tabia hii ilimfanya kukosa marafiki kutokana na watu wengi kupenda kupambwa kwa maneno ya uongo,” anabainisha na kuongeza;

No comments:

Post a Comment