Mwenyekiti
wa Taifa wa Shirikisho la vyuo vya Elimu ya juu Tanzania linaloundwa na
wanachama wa chama cha mapinduzi (CCM), Bi Zainabu Abdalah Issa akitoa
tamko la umoja huo lililolenga kuwakumbusha wanachama wa chama hicho
waliotangaza nia ya kuwania kuteuliwa kwenye nafasi ya Urais kuwa hakuna
aliye maarufu au mwenye nguvu kuliko chama bali mgombea wa chama hicho
atapatikana kwa mujibu wa taratibu na kanuni za chama na si vingenevyo.
Mwenyekiti
wa Taifa wa Shirikisho la vyuo vya Elimu ya juu Tanzania linaloundwa na
wanachama wa chama cha mapinduzi (CCM) Bi Zainabu Abdalah Issa akiwa na
wajumbe wa shirikisho hilo akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari
(hawapo pichani) wakati wa mkutano huo jijini Dar es salaam.
Shirikisho
la vyuo vya elimu ya juu Tanzania linaloundwa na wanachama wa Chama Cha
Mapinduzi limesema kuwa miongoni wa wanachama 42 walioomba kuteuliwa
kugombea urais kupitia chama hicho hakuna aliye maarufu au mwenye nguvu
kuliko chama hicho.
Hayo
yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa Shirikisho hilo Bi.
Zainabu Abdalah Issa wakati wa mkutano na vyombo vya habari.
“Shirikisho
la vyuo vya elimu ya juu tuna imani kubwa na wajumbe wote wa vikao
vyote vya maamuzi ndani ya chama chetu kwa kuwa watatuteulia mgombea
safi, muadilifu, na mzalendo atakayedumisha umoja na mshikamano ndani na
nje ya chama chetu”alisisitiza Zainabu.
Akifafanua
bi Zainabu amesema watia nia 42 wana Nafasi sawa katika uteuzi ambapo
ni jambo la wazi kuwa wapo watakaokidhi vigezo na wapo watakaoshindwa
kwa kuzingatia kanuni na taratibu za uteuzi ndani ya chama cha mapinduzi
(CCM).
Pia
Zainabu alitoa wito watia nia wote 42 kuwa mgombea atakayepitishwa na
vikao vyote vya maamuzi ndio atakuwa mgombea wetu wote na itakuwa ni
jukumu la kila mwanachama kumsemea na kumnadi kwa Watanzania wenzetu ili
CCM iendelee kuongoza Tanzania.
Akizungumzia
mfumo wa kutoa maamuzi ndani ya chama cha mapinduzi Zainab amesema kuwa
CCM ni Taasisi iliyoundwa kwa Muundo wa kuongoza kwa pamoja na kutoa
maamuzi kwa pamoja dhana inyodhihirisha kuwa Chama cha mapinduzi si mali
ya mtu binafsi au taasisi ya mtu mmoja inayotarajiwa kumfurahisha mtu
huyo.
Shirikisho
hilo linakipongeza chama hicho, kwa kuendelea kutekeleza demokrasia kwa
vitendo kwa kuwapa wanachama wake kushiriki kwenye nafasi zote za
uongozi ndani ya chama kwa ajii ya Uchaguzi Mkuu wa mwezi octoba 2015.
No comments:
Post a Comment