Waziri
wa Maliasili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akiteremka kwenye Coaster
mara baada ya kuwasili makao makuu ya ofisi za CCM Dodoma kwa ajili ya
zoezi la kuruisha fomu.
Baadhi ya
wanachama wa CCM waliomsindikiza Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro
Nyalandu, kurejesha fomu za kuomba kuteuliwa kuwania urais kwa tiketi ya
CCM mjini Dodoma, jana.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu amerejesha fomu za wadhamini
aliowapata katika mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani ambazo
ameziwasilisha makao makuu ya CCM mjini Dodoma na amesisitiza umuhimu wa
WanaCCM kumuunga mkono mgombea yeyote atakaeteuliwa na vikao vya
maamuzi na kuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM.
Waziri
Nyalandu akiongea baada ya kukabidhi fomu hizo kwa Naibu Katibu Mkuu wa
CCM, Rajabu Luhwavi, amesema hatuia ya kuungana WanaCCM wote baada ya
kupatikana kwa mgombea mmoja itakiwezesha chama kuimarika na amesisitiza
umuhimu wa kuendeleza misingi ya umoja na mshikamano iliyoachwa na
watangulizi wa nafasi ya Urais akiwemo Baba Wa Taifa Hayati Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akirejesha fomu za wadhamini
kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rajabu Luhavi, jana, baada ya
kukamilisha kazi ya kuomba udhamini kwa mikoa yote nchini.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na Naibu Katibu Mkuu wa CCM
(Bara), Rajab Ruhavi, wakihakiki fomu kabla ya kuzirejesha jana.
Mke
wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, Faraja, akisalimiana
na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rajabu Luhavi ofisini kwake katika
Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, wakati Nyalandu aliporejesha fomu zake
za kuomba kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM kwa nafasi ya urais.
WAZIRI
wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akisaini kitabu cha wageni
ofisini kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajabu Luhavi. Kulia ni mkewe
Faraja na kushoto ni Luhavi.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na mkewe Faraja, wakipongezwa
na sehemu ya umati uliojitokeza kwenye ofisi za Makao Makuu ya CCM mjini
Dodoma, wakati akirejesha fomu.
Picha ya pamoja.
No comments:
Post a Comment