Afisa
Masoko Bi.Kilave Atenaka akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi
waliotembelea kwenye banda hilo lililopo jirani ya kuingia katika banda
kubwa la Ukumbi wa Karume
Na Mwandishi Wetu
Taasisi
ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyochini ya Wizara ya Fedha
(UTT-PID) ipo kwenye Maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa ya
Dar-es-salaam, yanayoendelea katika mabanda ya Saba saba katika viwanja
vya Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa jijini.
Banda
la UTT PID lipo jirani na kuingia katika banda la Wizara ya fedha
upande wa kuingia kwenye banda la ukumbi wa Karume. Hivyo wamewaomba
wananchi mbalimbali wameombwa kujitokeza kupata huduma mbalimbali
zinazotolewa na taasisi hiyo ikiwemo huduma za uuzwaji wa viwanja
katika maeneo nchini ikiwemo vile vya mradi wa katika miji ya Chalinze
na Bagamoyo Mkoani Pwani.
Akielezea
Afisa Masoko Bi. Kilave Atenaka katika maonyesho hayo, alibainisha
kuwa mbali na uuzaji wa fomu kwa ajili ya viwanja, pia wanatarajia
kuanza kuuza kwa umma na taasisi mbalimmbali miradi mipya ikiwemo wa
Tundwi songani-Kigamboni jijini Dar es Salaam na ule wa Kingorwila
Mkoani Morogoro.
Aidha,
Bi Kilave alitumia wito huo kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi
ndani ya banda hilo kujipatia elimu mbalimbali zitolewazo na taasisi
hapa nchini.
Kwa
sasa UTT PID ni miongoni mwa taasisi zinazofanya vizuri katika utoaji
huduma za ushahuri katika maeneo ya upembuzi yakinifu wa miradi
mbalimbali, Uratibu wa fedha na huduma zinazohusiana katika maandalizi
ya mapendekezo ya miradi kwa benki au taasisi za fedha, uteuzi wa watoa
huduma kuhusiana na maandalizi ya zabuni na usimamizi wa majengo na mali
ambao ni utoaji wa huduma fanisi za usimamizi wa majengo yaliyochini ya
uangalizi thabiti wa taasisi.
Mmoja
wa wananchi aliyetembelea katika banda la UTT PID, akisaini kitabu cha
wageni wakati alipofika kujua shughuli mbalimbali za taasisi hiyo.
anayeshuhudia kulia kwa mwananchi huyo ni Afisa Masoko wa UTT PID,
Bi.Kilave Atenaka
baadhi
ya wananchi wakipata maelezo kutoka kwa Afisa Masoko wa UTT PID,
Bi.Kilave Atenaka wakati walipotembelea katika banda hilo..
No comments:
Post a Comment