Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
amemteua Mhandisi Edwin Amandus Ngonyani kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa
Shirika la Madini la Taifa (Stamico). Uteuzi huo umeanza Jumapili
iliyopita, Juni 28, 2015.
Taarifa
ya kuthibitisha uteuzi huo iliyotolewa Ikulu, Dar es salaam na Katibu
Mkuu Kiongozi (KMK) leo, Jumanne, Juni 30, 2015, inasema kuwa kabla ya
uteuzi wake Mhandisi Ngonyani alikuwa Mkaguzi Mkuu wa Migodi na Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Stamico.
Mhandisi
Edwin Ngonyani ni mhandisi wa migodini mwenye uzoefu wa muda mrefu wa
sekta ya madini. Anayo shahada ya kwanza ya fani hiyo kutoka Chuo Kikuu
cha Zambia na shahada ya uzamili (MSC) kwenye fani hiyo hiyo kutoka Chuo
Kikuu cha Exeter, Camborne School, Uingereza.
Mhandisi
Ngonyani amefanya kazi nzuri wakati anakaimu nafasi ya Ukurugenzi
Mtendaji na kwa kumteua, Rais Kikwete ana imani kubwa kuwa ataendeleza
kazi hiyo nzuri ya kuimarisha uwekezaji wa umma katika sekta hiyo ya
madini kupitia Stamico.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
30 Juni, 2015
No comments:
Post a Comment