Shirika la Utangazaji la Uingereza,
BBC limeelezwa kuwa baadhi ya wasichana waliotekwa na wanamgambo mjini
Chibok Nigeria wamekuwa wakishinikizwa kuwaua Wakristo.
Wanawake
watatu ambao wanasema walikuwa wakishikiliwa katika kambi moja na
wasichana hao wanasema wapiganaji wa BOKO HARAM waliwafunga mikono
wanaume wa Kikristo. Wasichana hao waliwachinja wanaume hao kwa kuwakata
shingo.Wanawake hao wanasema baadhi ya wasichana hao wa Chibok walikuwa na silaha. Baadhi ya wasichana waliwachapa mateka wengine wa kike. Haikuwa rahisi kuthibitisha ukweli wa taarifa hii. Wasichana 219 kati ya zaidi ya wasichana 270 waliotekwa kutoka shule moja ya bweni ya Chibok bado wanashikiliwa na Boko Haram.
No comments:
Post a Comment