SERIKALI imesema itawachukulia hatua kali wafanyabiashara wa mafuta,
ikiwamo kuwafungia vituo vyao na pia kufuta leseni zao watakaobainika
kugoma kuuza nishati hiyo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage amewaonya wamiliki wa vituo vya mafuta nchini wasije wakajiingiza katika mtego wa kufanya mgomo wa kuuza mafuta katika vituo vyao.
Mwijage alitoa tamko hilo wakati wa kipindi cha maswali na majibu ambapo Naibu Spika, Job Ndugai alimtaka atoe tamko la Serikali kutokana na taarifa zilizokuwa zikisambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwamba wauza mafuta wamepanga kugoma kuuza mafuta kuanzia leo ili kusubiri bei mpya ya bidhaa hiyo.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage amewaonya wamiliki wa vituo vya mafuta nchini wasije wakajiingiza katika mtego wa kufanya mgomo wa kuuza mafuta katika vituo vyao.
Mwijage alitoa tamko hilo wakati wa kipindi cha maswali na majibu ambapo Naibu Spika, Job Ndugai alimtaka atoe tamko la Serikali kutokana na taarifa zilizokuwa zikisambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii kwamba wauza mafuta wamepanga kugoma kuuza mafuta kuanzia leo ili kusubiri bei mpya ya bidhaa hiyo.
No comments:
Post a Comment